Wednesday, May 12, 2021

WAFANYAKAZI WA BENKI YA I&M WAMETOA MSAADA WA VITU MBALIMBALI KATIKA KITUO CHA WATOTO YATIMA – KIGAMBONI, DAR ES SALAAM.

 

Wafanyakazi wa Benki ya I&M wakiwa na baadhi ya watoto wa kituo hicho
Bi.Anitha Pallangyo, meneja masoko Benki ya I&M wapili kushoto akikabidhi baadhi ya zawadi walizopeleka kwenye kituo hicho cha watoto yatima
Timu ya Benki ya I&M leo walipotembelea kituo cha yatima chini ya mpango wao wa kujitolea wa 'IM for You' kushoto ni Bi. Hellen Mbwana, afisa wa benki kitengo cha ukaguzi, Anitha Pallangyo, meneja masoko, Mlekwa Augustine, huduma kwa wateja, Theresia Nguma kitengo cha malipo, fedha na biashara, na Debora mwakyoma afisa masoko na mawasiliano ya benki.

 Timu ya wafanyakazi wa I&M walipotembelea kituo cha watoto yatima cha Lady Fatema kilichopo Mjimwema mageti saba, kigamboni Jijini Dar es salaam.

DAR ES SALAAM. Wafanyakazi wa Benki ya I&M Tanzania siku ya Jumanne tarehe 11, Mei, 2021, wamejitolea msaada wa vitu mbalimbali kama vile vyakula, nguo, sabuni pamoja na vifaa vya shule katika moja ya kituo cha kulea watoto yatimakiitwacho ‘Lady Fatema’  kilichopo Mjimwema mageti saba, Kigamboni Jijini Dar es salaam chini ya mpango wao wa ‘IM FOR YOU’ katika jitihada za kurudisha kwa jamii kupitia mpango huo ambapo wafanyakazi hujitolea kwa jamii kwa njia mbalimbali kama vile kutoa elimu ya fedha na ujasiriamali kwa wanawake na vijana ili waweze kujiajiri pamoja na kusaidia vitu mbalimbali kwa wahitaji.

Wasimaizi wa kituo hicho Bi. Mariam Ramadhan na mmewe Bw. Kalekela Omari Mahmood walianzisha kituo hicho mnamo mwaka 2011 wakiwa na lengo la kusaidia watoto yatima wanaoishi katika mazingira hatarishi wakiwapatia elimu, chakula na hifadhi ya kulala. Mbali na misaada mbalimbali inayopelekwa na wafadhili, kituo hicho kina changamoto ya eneo la kutosha la kuweza kuhifadhi watoto wengi na wa jinsia tofauti kwani kwa sasa imewalazimu kubaki na jinsia ya kiume tu kutokana na ukosefu wa vyumba vya kutosha kwaajili ya watoto hao.

Katika kuadhimisha mwezi mtukufu wa Ramadhani na ikiwa ni wiki ya kuelekea sikukuu ya Eid Al-Fitr, wafanyakazi wa benki ya I&M waliamua kujitolea vitu hivyo katika kituo cha kulea watoto yatima Mjimwema Kigamboni ili na wao waweze kusheherekea na kufurahia sikukuu ya EID inayotarajiwa kuwa mwishoni mwa wiki hii kutegemeana na kuandama kwa mwezi. Vilevile wafanyakazi wa benki ya I&M waliweza kuwapa elimu ya usimamizi wa fedha na ujasiriamali kwa vijana na wanawake waliokuwa katika kituo hicho ili iweze kuwasaidia katika usimamizi wa fedha za kituo hicho pamoja na kijiajiri wao wenyewe pindi watakapoanza kujitegemea.

Benki ya I&M kupitia wafanyakazi wake wameweza kufanya kampeni mbalimbali za kusaidia jamii kama vile kujitolea kwa kufundisha wanawake, vijana na wajasiriamali katika kikundi cha Wanawake wajasiriami kilichopo Yombo vituka, Temeke jijini Dar es salaam, vilevile wiki iliyopita wafanyakazi wa benki hiyo walijitolea damu  ili kusaidia wagonjwa wenye uhitaji wa damu katika hospitali ya Taifa ya Muimbili.

Monday, May 3, 2021

I&M Holdings PLC Completes Acquisition of Orient Bank Limited in Uganda

 


 Nairobi/Kampala, 3rd May, 2021: I&M Holdings PLC has announced the majority acquisition of Orient Bank Limited (OBL) from 8 miles LLP and Morka Holdings Limited. OBL is the 12th largest bank and a licensed and established commercial bank in Uganda.
I&M Holdings PLC and Orient Bank Limited signed an agreement in July 2020 for I&M Holdings PLC to acquire 90 percent shareholding of the Ugandan entity. The acquisition was completed on 30th April 2021 after receiving the necessary approvals from the Central Bank of Kenya, Bank of Uganda, Capital Markets Authority of Kenya and the COMESA Competition Authority.
The move underscores I&M Group’s commitment to its growth and expansion strategy in Eastern Africa, where Uganda was the missing link in the Group’s strategic effort to set up its presence in all East African countries.  A key focus of this strategy is to seek opportunities to invest at a local and regional level enabling the Bank to serve the needs of all customers, while promoting trade flows within the region.
This development supports the Group’s Business Growth initiatives through diversification of revenue streams by entry into new markets and extension of its Corporate, Business, Personal Banking, as well as Treasury and Trade Finance solutions, to all its customers operating in Uganda.
Commenting on the acquisition, I&M’s Group Executive Director, Sarit Raja Shah noted, “I&M Group aspires to be Eastern Africa’s leading financial partner for growth.  The acquisition of OBL will place I&M Bank in an advantageous position to capitalise on the growth in the Eastern African economies and thereby ultimately increasing shareholder value.”
“This acquisition is expected to give the Group greater capacity to grow profitably, through extending our network to our Regional customers. Further it demonstrates our continued leadership role in the industry across East Africa”, Sarit Raja Shah added.
Dr. Ketan Morjaria, a founding member of OBL and continuing shareholder and Director said “This acquisition marks a great milestone in the history of Orient Bank. We are proud to be integrating into a regional group like I&M Holdings PLC and this synergy will allow our customers to benefit from more seamless and superior banking products whilst continuing our tradition of trust.”
Kumaran Pather, CEO of OBL said “The acquisition of OBL into I&M Holdings PLC will see the new entity rise to greater heights and allow us to broaden our market reach and penetration. The management of OBL are excited to be part of a large and
fast growing Group and look forward to serving new and existing customers alike with better products, digital platforms and regional services.”    
Through the acquisition, I&M Group has acquired additional net loan assets of approximately KES 7.7 Billion, deposits of KES 18.2 Billion, a customer base of close to 70,000, a staff component of 340 employees and a network of 14 branches and 22 ATMs across the country.
A clear plan for the integration of OBL has been developed and through its execution the Group expects to gain considerable business and operational synergies.
I&M Group has made significant investments in its robust infrastructure as part of its digital transformation journey. Through this acquisition, OBL customers will now benefit from this technologically driven infrastructure, which will give them a wide suite of market driven financial solutions aimed at meeting their financial and lifestyle requirements.  
The I&M Group will continue to focus on mergers and acquisitions as part of its growth strategy, as we continue to enhance our shareholders’ value and to provide our customers with a wide network of banking solutions across the region.
The transaction with OBL adds to a list of previous strategic alliances that the Group has effectively completed such as the acquisition of Giro Commercial Bank Limited in Kenya, I&M Burbidge Capital Limited in Kenya and Uganda, CF Union Bank in Tanzania, BCR Bank in Rwanda and First City Bank in Mauritius. We believe that our aspiration in becoming Eastern Africa’s leading financial growth partner is well on course.
In his concluding remarks, Mr. Sarit Raja Shah, noted, “Uganda has made great strides in improving access to financial services across the country. The partnership with Orient Bank Limited is very timely since the Group plans to play a significant role in the growth of the banking sector in Uganda, as it has done in other East African markets.”

Saturday, May 1, 2021

WAFANYAKAZI WA I&M BANK WAJITOLEA DAMU KUOKOA MAISHA YA WATANZANIA WAKISHIRIKIANA NA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

 

Meneja masoko na mawasiliano benki ya I&M Tanzania kushoto Bi.Anitha Pallangyo akiwa na wafanyakazi wenzie katika kampeni ya uchangiaji dau
         Damu ikiendelea kutolewa kutokana na hamasa iliyoletwa na wafanyakazi wa Benki ya I&M
    Bi.Lencer Odhiambo kutoka kitengo cha huduma kwa wateja cha benki ya I&M akiwa anajitolea damu katika kampeni ya kuchangia damu   
    Mkuu wa kitengo cha mikopo Bw.Clemence Kagoye wa benki ya I&M akiwa anatoa damu katika kampeni ya kuchangia damu ilioandaliwa na benki hiyo

Mwandishi Wetu

Benki ya I&M Tanzania, Ijumaa tarehe 30 Aprili 2021, walifanya Kampeni ya utoaji Damu ili kuokoa maisha ya watanzania chini ya mpango wao wa ‘IM FOR YOU’ katika jitihada za kurudisha kwa jamii. Kampeni hiyo ilifanyika Makao Makuu ya Benki hiyo yaliopo Maktaba Square jijini Dar es salaam.

Zaidi ya wafanyakazi 30 walishiriki na kujitolea Damu ili kuiwezesha Serikali kukabiliana na upungufu wa Damu kupitia hospitali ya taifa ya Muhimbili ambayo ilishirikiana na Benki hiyo katika zoezi la utoaji damu.

Kwasababu uhitaji wa damu bado upo, Benki ya I&M kupitia mpango wake wa ‘IM FOR YOU’ ambao wafanyakazi wake hujitolea kwa jamii wameamua kufanya kampeni hii ya uchangiaji damu kama njia ya kurudisha kwa jamii.

Akiongea wakati wa zoezi hilo la kujitolea damu, Bi. Anitha Pallangyo, Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya I&M alisema,”tumefurahishwa sana na muitikio ambao wafanyakazi wenzetu wameonyesha katika zoezi hili la kipekee. Tunawashukuru sana hospitali ya Taifa  Muhimbili kwa muitikio wao walioonyesha kwa kukubali kushirikiana nasi katika zoezi hili la utoaji damu ili kuokoa maisha ya watanzania wengi wenye uhitaji wa damu.”

 Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Kitengo cha Uboreshaji huduma za Benki Bi. Deepali Ramaiya, , Alisema “Hii ni moja ya mipango mikakati ya aina yake ambayo huanzishwa  na wafanyakazi wenyewe wa Benki ya I&M, kwa kujitolea huduma bure kwa jamii kama vile kutoa Elimu ya Ujasiriamali bure kwa wafanyabiashara kupitia Vikundi mbalimbali na sasa wamejitolea damu kupitia Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

 Naye Afisa muhamasishaji damu kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,John Daniel Bigambalaye alisema, “sisi kama wawakilishi wa Muhimbili kitengo cha damu, tumehamasika na kampeni hii iliyoandaliwa na wafanyakazi wa Benki ya I&M kwa jitihada hizi za kusaidia hospitali ya Taifa na watanzania wenye uhitaji wa damu kwa ujumla. Tunashauri na taasisi nyingine ziwe mstari wa mbele katika kuhamasisha wafanyakazi wake kujitolea kwa jamii”

 Benki ya I&M kupitia wafanyakazi wake wameweza kufanya kampeni mbalimbali za kusaidia jamii kama vile kujitolea kufundisha Wanawake, Vijana na Wajasiriamali, kujitolea damu  na mengine mengi kwenye sekta ya Afya, Elimu na Mazingira.

 Licha ya wafanyakazi wa Benki ya I&M kujitolea damu pia walialika Taasisi mbalimbali na kampuni zilizo karibu na Makao Makuu ya Benki ili kushiriki.

Tuesday, April 27, 2021

KAMATI YA MAKATIBU WAKUU YAANDAA MKAKATI KABAMBE WA KUBORESHA MICHEZO MASHULENI

 


Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara zenye dhamana yaElimu,Michezo na TAMISEMI  wakiwa kwenye kikao kazi leo Aprili 27,2021 Jijini Dodoma kujadili utekelezaji wa maelekezo ya Mawaziri wenye dhamana hizo hizo kwa lengo la   kuandaa Mkakati wa Utekelezaji wa masuala mbalimbali ya uimarishaji wa somo la Elimu kwa Michezo na Michezo katika shule za Msingi na Sekondari hapa nchini chini ya uenyekiti wa Prof.Riziki Shemdoe ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya  TAMISEMI.


Dkt. Hasssan Abbasi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia eneo la Elimu ndugu  Gerard Mweli (kulia) wakihudhuria kikao cha Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara zenye dhamana ya Elimu, Michezo na TAMISEMI  wamefanya kikao kazi leoAprili 27,2021Jijini Dodoma kujadili utekelezaji wa maelekezo ya Mawaziri wenye dhamana hizo hizo kwa lengo la   kuandaa Mkakati wa Utekelezaji wa masuala mbalimbali  yauimarishaji wa somo la Elimu kwa Michezo na Michezo katika shule za Msingi na Sekondari hapa nchini. Upande wa pili ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Yusufu Omary Singo

 

Na John Mapepele, Dodoma

Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara zenye  dhamana ya Elimu, Michezo na TAMISEMI  wamefanya kikao kazi leo Aprili 27,2021 Jijini Dodoma kujadili  utekelezaji wa maelekezo ya Mawaziri  wenye dhamana hizo hizo kwa lengo la   kuandaa  Mkakati  wa Utekelezaji wa masuala  mbalimbali  ya uimarishaji wa somo la Elimu kwa Michezo na Michezo katika shule za Msingi na Sekondari  hapa nchini

Mwenyekiti wa Kikao hicho, Prof. Riziki  Shemdoe  ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI amesema  miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa  na kukamilika ni pamoja na   kuandaliwa kwa  mapendekezo ya uimarishaji wa ufundishaji wa somo la michezo shuleni na tahasusi zenye somo hilo kwa kidato cha tano  ambapo ameseme tahasusi hizo zitaanza kufundishwa katika mwaka huu wa masomo.

Pia rasimu ya Mpango Mkakati na Mikakati ya utekelezaji wa masuala mbalimbali ya  somo  la Elimu kwa michezo na michezo katika shule za Msingi na Sekondari  imeandaliwa ili  kuboresha  michezo mashuleni.

Kuhusu kuandaa kiunzi cha uendeshaji wa michezo ya UMITASHUMTA na UMISSETA  Prof. Shemdoe amesema  tayari  Kamati ya Wataalam imeshauri kuwa  kwa sasa  miongozo iliyopo itumike na kiunzi tayari kimeshaandaliwa kwa kuzingatia changamoto  zilizopo ambapo  kitajadiliwa  na wadau wote Juni mwaka huu wakati wa michezo ya UMISHUMTA NA UMISSETA na  kwa sasa tayari miongozo hiyo imeshatumwa kwenye  mikoa yote hapa nchini.

Aidha, suala la uundwaji wa Kamati ya kitaifa ya UMISHUMTA NA UMISSETA tayari imependekezwa na kukubalika kuundwa kwa Kamati ya Usimamizi itakayoundwa na wataalam wawili wawili kutoka kwenye kila Wizara ambapo imekubalika kuwa  pamoja na usimamizi, Kamati itatumia fursa hiyo kujifunza na kuangalia changamoto zilizopo kwenye uendeshaji wa michezo ya UMITASHUMTA  na UMISSETA kuandaa  mapendekezo yatakayojadiliwa  na wadau wote kwa ajili ya  maboresho zaidi.

Prof. Shemdoe amesema kuhusu mchakato wa maandalizi ya UMISHUMTA NA UMISSETA mwaka huu, tayari mikoa yote imeshaandikiwa barua ya taarifa na Mhe. Waziri Ofisi ya Rais –TAMISEMI na kwamba waratibu wa michezo wanakwenda kwenye ukaguzi wa viwanja na maeneo ya malazi na chakula kuanzia Aprili 28-30, mwaka huu. Pia Kamati ya wataalam inaendelea na ufuatiliaji wa Shule teule za michezo ili kuhakikisha kuwa michezo inafanyika kwenye kiwango kinachotakiwa.

Makatibu Wakuu walioshiriki  kwenye  kikao hiki ni pamoja Mwenyekiti wa kikao hicho, Prof. Riziki  Shemdoe  ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI,na Naibu wake  anayeshughulikia eneo la Elimu ndugu  Gerard Mweli, mwingine ni  Dkt. Hasssan Abbasi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Dkt. Leonard Akwilapo  kutoka  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojioa pamoja na Watendaji mbalimbali kutoka  Wizara hizo.

Maelekezo  ya Mawaziri wenye dhamana ya elimu, Michezo na TAMISEMI yalitolewa wakati wa kikao cha pamoja kilichofanyika Februari 8, Mwaka huu.

Tuesday, April 20, 2021

SERIKALI YAANZISHA KITUO CHA KIMATAIFA CHA KUENDELEZA VIPAJI VYA MICHEZO.

 


 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini, Yusuph Singo Omari (kushoto), akiwa naa liyewahi kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF na Kocha wa Timu ya Taifa Stars, Ami Ninje (katikati) na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya Dkt. Richard Masika wakikagua eneo la chuo kwa ajili ya mradi wa upanuzi wa chuo hicho ili kujenga Kituo cha kuendeleza vipaji vya michezo.

Timu ya wataalam mbalimbali wa michezo na ardhi ikipitia ramani ya maeneo ya ujenzi wa madarasa na hosteli.

Timu ya wataalam ikiangalia eneo la ujenzi wa madarasa wa Kituo cha kuendeleza vipaji vya Michezo

 



Na John Mapepele, Dodoma

 

Serikali inatekeleza mradi wa  kupanua eneo la  Chuo cha  Maendeleo ya Michezo Malya ikiwa ni  mkakati  maalum wa kuanzisha Kituo cha Kuendeleza Vipaji vya Michezo  ili kuibua na kuendeleza vipaji vya wanamichezo hapa nchini.

 

Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini, Yusuph Singo Omary ameyasema haya  wakati alipokuwa na  Timu ya wataalam walipotembelea na kukagua eneo  hilo hivi karibuni ikiwa ni sehemu ya kufanya maandalizi ya ujenzi wa kituo hicho ambacho kitakuwa na hadhi ya kimataifa.

 

“Niseme tu kwamba  kukamilika kwa kituo  hiki kutaifanya  nchi yetu kusonga mbele kwenye  Sekta ya Michezo kwa kuwa  vipaji vya wanamichezo wetu vitaibuliwa na  tutaweza sasa  kushindana  na mataifa mengine duniani sasa” amefafanua Mkurugenzi Omary

 

Amesema Tanzania ina hazina kubwa ya vipaji kilichokuwa kinakosekana ni kituo maalum cha michezo cha kuwanoa wachezaji na kwamba kukamilika kwa kituo hiki ni suluhisho la kudumu la changamoto hiyo.

 

Awali, Katibu Mkuu wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi amesema  Wizara imeendelea  kufanya mageuzi makubwa ili kutimiza ahadi  za Serikali na matarajio ya wananchi kwa ujumla.

 

Amesema Wizara  inatekeleza kwa kwa kasi  masuala yote  yaliyobainishwa kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka  2020-2025 ikiwemo ibara125(a)-(h) kwa Sekta ya Habari, ibara239 (a)-(m) kwa Sekta ya Utamaduni, ibara 249 (a)-(j) Sekta ya Sanaa na ibara 243(a)-(k) kwa Sekta ya Michezo.

 

Akihutubia kwenye kikao cha Wafanyakazi wa wa Wizara hiyo hivi karibuni, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa amesema tayari Wizara yake imeshakamilisha agizo la Serikali la kuanzisha Mfuko wa Sanaa na Utamaduni ikiwa pia ni mkakati wa kukuza sekta ya Michezo nchini.

 

“Wizara imekamilisha agizo hili kwa kuhuisha Mfuko wa Maendeleo ya Sanaa na Utamaduni ambao umetengewa shilingi bilioni 1.5. 

Mfuko  huu kwa  mwaka ujao wa fedha utajikita katika ujenzi wa miuondombinu muhimu ikiwemo jengo la SANAA HOUSE hapa Dodoma, pia utaendelea  kutengewa fedha zaidi kwa lengo la kutekeleza  majukumu mawili adhimu; kuwajengea uwezo wanatasnia hizo za Sanaa na Utamaduni kupitia mafunzo na  kuwawezesha kupata mikopo na ruzuku katika kazi zao” amesisitiza Waziri Bashungwa

Wednesday, April 14, 2021

MAWAZIRI WATEKELEZA AGIZO LA RAIS SAMIA SULUHU KIKAMILIFU

 


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Pauline Gekul (kushoto) akizungumza leo katika kikao cha Mawaziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na Wizara hiyo cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu ya Sekta hizo ya kisera, kisheria na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchini kilichofanyika jijini Dodoma, anayefuata ni Waziri wake Innocent Bashungwa akifuatiwa na Waziri waMawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Faustine Ndugulile na kuliani Naibu wake Mhandisi Kundo Mathew.

Kikao hicho kimefanyika kufuatia maelekezo yaliyotolewa hivi karibuni na Mheshimiwa  SamiaSuluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  yakutaka kufanyika marekebisho ya Sheria na Kanuni zinazosimamia Vyombovya Habari  hapa nchini hususan Televishen Mtandao (Online TV)

 

Wajumbe wa kikao cha Mawaziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja naWizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbas akizungumza katika kikao hicho cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu yaSekta hizo ya kisera, kisheria  na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchini kilichofanyika jijini Dodoma leo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbas (kushoto), akifuatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Zainab Chaula akifuatiwa na Naibu wake Dkt. Jim Yonaz katika kikao cha Mawaziri wa Wizara hizo mbili cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu ya Sekta hizo ya kisera, kisheria na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchin ikilichofanyika jijini Dodoma leo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbas (kushoto) akizungumza leo katika kikao cha Mawaziri wa Wizara hiyo na Wizara ya Mawasiliano naTeknolojiaya Habari cha kujadili hoja zinazohusu utekelezaji wa majukumu ya Sekta hizo yakisera, kisheria na kikanuni kwenye masuala ya mawasiliano nchini kilichofanyika jijini Dodoma.Kulia ni Katibu Mkuu waWizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Zainab Chaula. Kikao hicho kimefanyika kufuatia maelekezo yaliyotolewa hivi karibuni na Mheshimiwa SamiaSuluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yakutaka kufanyika marekebisho ya Sheria na Kanuni zinazosimamia Vyombo vya Habari hapa nchini hususani Televishen Mtandao (Online TV)

 

Na John Mapepele, Dodoma

Waziri anayesimamia Sekta ya Habari Mhe. Innocent Bashungwa na Waziri anayesimamia Sekta ya Mawasiliano Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile na timu ya Makatibu  Wakuu na Wataalam  wa Wizara hizo  wamekaa na kujadili  hoja mbalimbali kuhusu  utekelezaji wa Sera, Sheria na Kanuni za kisekta kufuatia  maelekezo  ya hivi karibuni ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Maelekezo hayo aliyatoa   wakati wa  kuwaapisha Makatibu Wakuu, Naibu  Makatibu  Wakuu na  Wakuu wa Taasisi ya kufanya marekebisho ya Sheria na Kanuni  zinazosimamia Vyombo vya Habari hususan Televisheni Mtandao (Online TV).

Majadiliano hayo yamefanyika jijini Dodoma Aprili 14, 2021 na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa kwenye hoja 13 zilizoainishwa na Wizara hizo.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Innocent Bashungwa  amesema miongoni mwa  maazimio  yaliyofikiwa ni pamoja na kufanya  mapitio ya Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo katika maeneo yote yenye mapungufu  ili ziendane na  hali halisi ya sasa  na  kuweka  mifumo rafiki ya kushughulikia masuala  yote  yanayohusu sekta ya  Mawasiliano na Utangazaji

“Tumeagiza Wataalam wafanye uchambuzi wa Kanuni za Maudhui Mtandaoni ili kuona kama zinaendana na mazingira ya sasa” amesisitiza Waziri Bashungwa

Ameongeza kuwa Wizara zimeaazimia kuja na mkakati wa kuwaelimisha  wadau wa Sekta hizo ili kudhibiti makosa  ya kimaudhui  yanayofanywa  na Vyombo vya Habari badala ya hali ilivyo sasa inayotoa adhabu kali zinazojikita kwenye utozaji wa faini kubwa pamoja na kufungiwa.

Suala lingine ambalo limeazimiwa kufanyiwa kazi ni chaneli za bure kutoonekana kwenye visimbusi ambavyo kimsingi zinapaswa kuonekana hata pale kifurushi kinapokuwa kimeisha muda wake.

Kwa upande wake Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine  Ndugulile amesema kukua kwa teknolojia kumewezesha kukua kwa matumizi ya huduma za mawasiliano yakiwemo ya utangazaji hivyo katika kipindi kifupi  kijacho Serikali  kupitia  Wizara hizo mbili  itafanya  maboresho  makubwa  kwenye kanuni husika ili kuendana na  hali halisi ya sasa.

 

Ameongeza kuwa Serikali ilitunga Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali zikiwemo Sheria ya huduma za Habari Namba 12 ya mwaka 2016, Sera ya Habari na Utangazaji ya mwaka 2003 na Sera ya Taifa ya TEHAMA ya mwaka 2016 ambazo pamoja na mambo mengine zinaelekeza kuweka mazingira wezeshi ya kukuza maudhui ya ndani (Local content).

Thursday, April 8, 2021

MHE GEKUL AOMBA USHIRIKIANO BAINA YA VIONGOZI WAKUU WA WIZARA,WATENDAJI NA WATUMISHI

 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Innocent Bashungwa (katikati mwenye tai nyekundu) akiwa  na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt Hassan Abbasi (mwenye tai ya bluu) wakimkaribisha Naibu Waziri, Mhe. Pauline Gekul alipowasili rasmi kwenye Ofisi yake mpya iliyopo eneo la Mji wa Serikali –Mtumba jijini Dodoma leo, baada ya kuapishwa  na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Aprili 01,2021 Ikulu ya Chamwino  kushika wadhifa huo.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Pauline Gekul akipokea maua kutoka  kwa wafanyakazi wa Wizara hiyo  kama ishara ya kumkaribisha rasmi kwenye Ofisi yake mpya iliyopo  eneo la Mji wa Serikali –Mtumba jijini Dodoma leo, baada ya kuapishwa  na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Aprili 01,2021 Ikulu ya Chamwino  kushika wadhifa huo

a.    Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Pauline Gekul akisaini  kitabu  cha wageni  mara baada ya  kuingia kwenye Ofisi yake mpya iliyopo eneo la Mji wa Serikali –Mtumba jijini Dodoma leo, baada ya kuapishwa  na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Aprili 01,2021 Ikulu ya Chamwino  kushika wadhifa huo.

                                     

Na John Mapepele, Dodoma


Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Philipo Gekul ameomba ushirikiano baina Viongozi Wakuu wa Wizara, Watendaji na Watumishi wote wa Wizara ili kutekeleza majukumu ya Wizara hiyo kimamilifu kulingana na Miongozo ya Serikali, Maelekezo ya Mheshimiwa Rais na Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) hatimaye matarajio ya wananchi yaweze kufikiwa.



Mhe. Gekul ameyasema haya alipowasili rasmi leo kwenye Ofisi yake mpya eneo la Mji wa Serikali- Mtumba jijini Dodoma mara baada ya kuteuliwa na Mheshimiwa Rais kwenye nafasi hiyo hivi karibuni akitokea Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambako alikuwa akihudumu kwa nafasi hiyohiyo.



“Mheshimiwa Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara, madaraka haya tuliyopewa ni sawa na makoti ya kuazima hivyo tuna kila sababu ya kumtanguliza Mungu na kuimarisha ushirikiano ili kuleta matokeo tarajiwa kwa wananchi wetu wakati tunatekeleza majukumu yetu ya kila siku” amesisitiza Mhe. Gekul

Amemshukuru Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumwamini na kumrejesha tena kwenye nafasi hiyo pamoja na viongozi wote Wakuu wa Wizara hiyo ambapo ameongeza kuwa hali hiyo itarahisisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa ufanisi kwa kuwa watendaji wote wamerejeshwa na wanauzoefu wa kutosha.

Amemhakikishia Waziri Bashungwa kufanya kazi kwa bidii ya kumshauri na kumsaidia kwa kadiri ya uwezo wake wote kama msaidizi wake.

Kwa upande wake, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa amesema Watumishi wote kuwa na mshikamano wa hali ya juu ambapo amesisitiza watumishi wasisubiri kusukumwa na Katibu Mkuu na badala yake wachape kazi ili kukidhi dhamira ya Mhe. Rais ya kuwatumikiwa wananchi kikamilifu.

“Napenda kusema tukigundua mahali popote kwenye Wizara yetu hakuna ushirikiano tutachukua hatua mara moja maana hiyo itakuwa ni hujuma kwa taifa”amefafanua Mhe. Bashungwa

Amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa kumwamini na kumteua tena kuendelea kusimamia Sekta zilizo chini ya Wizara hiyo pia kumteua Mhe. Gekul kuja kuongeza nguvu katika kutekeleza na kumuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kutekeleza Ilani ya CCM na hotuba aliyoitoa awali kama mwongozo kwa Watendaji wote wa Serikali.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi amemshukuru Mhe.Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kumwamini na kumteua kwa mara nyingine kuwa Katibu Mkuu na kumwahidi kushirikiana na Viongozi na Watumishi wote kutekeleza majukumu ya Wizara kwa weledi na kuzingatia taaluma.

Akizungumza kwenye Kikao cha Menejimenti ya Wizara hiyo mara baada ya kupokea maelekezo ya Waziri Bashungwa, Dkt. Abbasi amesisitiza watendaji wa Wizara kutoka na kuwa jirani na wadau wa sekta zilizochini ya Wizara hiyo kwa kuwa wanahitaji kulelewa kwa karibu.

Amesema jukumu la Wizara ni kuzisimamia sekta zilizo chini ya wizara hiyo kikamilifu kwa weledi ili kupata matokeo chanya kwa kuwa nchi yetu imebahatika kuwa na wasanioi wenye vipaji na vipawa vingi kinachotakiwa ni usimamizi madhubuti.